Ufunguzi
wa tukio la kuzindua simu ya TECNO CAMON 19
Dar
es Salaam, Tanzania, 06 Julai, 2022-
TECNO Mobile Tanzania, chapa ya simu za kisasa na bora duniani ambayo imekuwa
ikitoa teknolojia ya kisasa zaidi kwa watumiaji, leo imetangaza uzinduzi wa
toleo lake la CAMON 19 kwa kushirikiana na Vodacom. Toleo la CAMON 19 limekuja
ili kukabiliana na changamoto za kitamaduni zinazohusishwa na upigaji picha
wakati wa usiku na hali ya mwanga hafifu, ikiwa na vipengele kama vile
teknolojia ya upigaji picha za usiku ya 64MP na bezel ndogo zaidi ya 0.98mm ya
tasnia.
TECNO
na Vodacom wanaungana kuhakikisha wanawapatia wateja wao simu ya kisasa yenye
kifurushi cha intaneti cha 96GB BURE kwa muda wa mwaka mzima ili sio tu kuinua
ujuzi wao wa kupiga picha, bali pia kuwasaidia kuhamia katika ulimwengu wa
kidijitali.
Akizungumza
wakati wa uzinduzi huo, Afisa Uhusiano wa TECNO Bi. Prisca Ernest
alisema, "Tunajivunia kutambulisha toleo jipya la CAMON 19 na
kuendelea kuimarisha dhamira yetu ya kukua na kuwekeza zaidi katika nyanja za
teknolojia na ubunifu."
Afisa
uhusiano wa TECNO akizungumza kuhusu sifa kuu za CAMON 19
Bi
Prisca alisisitiza zaidi juu ya teknolojia ya upigaji picha za usiku, alisema,
"Simu yetu ya CAMON 19 inakuja na kamera kuu ya 64MP na sensor ya RGBW /
glasi. Kamera hii ya CAMON 19 imeleta viwango vipya vya kupiga picha angavu na
halisi hata nyakati za usiku.
Aliongeza
pia,” TECNO CAMON 19 ina bezel nyembamba sana ya 0.98mm, ikiwa na skrini ya
inchi 6.8 FHD+ inayotoa uzoefu usio na kifani.”.
Zaidi
ya hayo, alisema kuwa TECNO CAMON 19 Pro inaendeshwa na chipset ya MediaTek
Helio G96 yenye skrini bora, nguvu zaidi ya kuchakata picha na kasi ya juu
zaidi.
Pia
alitaja vipengele vingine vya kuvutia vya CAMON 19 ikiwa ni pamoja na muundo
maridadi, nafasi kubwa ya 256+8GB na 120Hz.
Sifa
kuu za simu ya TECNO CAMON 19
Afisa Mkuu wa Biashara wa TECNO, Bi. Salma Shafii, alisema, “Lengo la kushirikiana na Vodacom ni
kukuza maisha ya kidijitali katika jamii ya Watanzania, kuongeza idadi ya simu
za kisasa na watumiaji wa intaneti sokoni kupitia uzinduzi wa vifaa vya simu
kama vile toleo jipya la CAMON 19”.
Bi
Salma aliongeza kuwa, “Nina furaha kutangaza kwamba kila mteja atakayenunua
TECNO CAMON 19 atapata intaneti ya mwaka 1 bure ya GB 96 kutoka Vodacom na
zawadi nyingine za papo kwa hapo ikiwemo spika ya Bluetooth, power bank na
tiketi ya sinema kutoka Century Cinemax.”
Afisa
mkuu wa Biashara wa TECNO akizungumza kuhusu faida za kununua simu ya TECNO
CAMON 19
Vile
vile, meneja wa masoko wa TECNO Bw. William Motta, alisema,
“Toleo la CAMON 19 limekuja katika aina tatu za ambazo ni CAMON 19, CAMON 19
Pro na CAMON 19 Pro 5G. Bei zitakuwa 450,000 kwa CAMON 19 (128+4GB), 510,000
kwa CAMON 19 (128+6GB), 660,000 kwa CAMON 19 Pro, na 790,000 kwa CAMON 19 Pro
5G.
Tembelea
duka lolote la TECNO au duka la Vodacom ili kupata uzoefu wa simu hii mpya. Pia
unaweza kuagiza mtandaoni kupitia INALIPA: https://www.inalipa.co.tz/stores/tecno#/
Kwa maelezo zaidi piga simu namba 0744 545 254 au 0678
035 208.