Je, Unatafuta Kazi au Ajira?
<< BOFYA HAPA>> Kupata Ajira Yako Leo

Thursday, July 14, 2022

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo July 14

Read More

Wednesday, July 13, 2022

Rais Samia Aridhia Wadaiwa Sugu Kodi Ya Ardhi Kusamehewa Riba


Na Munir Shemweta, SERENGETI
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameridhia kusamehewa riba ya kodi ya pango la ardhi kwa wadaiwa sugu kwa masharti kwamba wadaiwa hao wawe wamelipa  madeni ya msingi ndani ya miezi sita kuanzia mwezi julai hadi desemba 2022.

Hayo yamebainishwa tarehe 12 Julai 2022 na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula katika mkutano na wananchi wa kijiji cha Nyachoka wilayani Serengeti mkoani Mara wakati wa zoezi la kukabidhi hati miliki za kimila.

Jumla ya hatimiliki za kimila 6,155 zimekamilika na kutolewa kwa wananchi wa vijiji 22 katika wilaya ya Serengeti ambapo hati 1621 sawa na asilimia 26 zimekamilishwa kwa ajili ya akina mama  na hatimiliki 1519 sawa na asilomia 25 ni za umiliki pacha kati ya wanaume na wanawake.

Dkt Mabula alisema yeye pamoja na Waziri wa Fedha ambaye ndiye mwenye dhamana ya kusamehe watakutana na kupanga namna bora ya kutekeleza msamaha huo.

“Najua kuna wengi wanadaiwa madeni ya muda mrefu kwa hiyo kumetokea msamaha kuanzia mwezi julai mpaka desemba mwaka huu, watakaoweza kulipa ndani ya miezi hii sita, wale ambao madeni yao yana miaka mitano kurudi nyuma watalipa bila ile tozo ya riba” alisema Dkta Mabula.

” Mhe mama samia ameridhia kupitia waziri wa fedha kwa kushirikiana na waziri wa ardhi waweke utaratibu mzuri wa ninyi kuondolewa tozo ile na msamaha ni wa miezi sita tu kama una ndugu mpigie simu mwambie serikali ya awamu ya sita chini ya mama samia imetoa msamaha kwa wadiwa sugu ili watoke katika jina baya la wadaiwa sugu kwenda kulipa madeni bila riba” alisema Dkt Mabula

Kwa mujibu wa Waziri wa Ardhi, mmiliki wa ardhi atakayeshindwa kulipa madeni yake katika kipindi cha miezi hiyo sita basi atadaiwa madeni yake pamoja na riba na akishindwa kufanya hivyo atafikishwa kwenye vyombo vya sheria ambako huko uamuzi wake ni kulipa ama kunyang’anywa ardhi anayoimiliki.

Akigeukia zoezi la utoaji hatimiliki za kimila Dkt Mabula alisema, hatua ya kumilikishwa ardhi kwa nyaraka kuna faida kubwa katika maisha ya kila siku na kutaja baadhi ya faida hizo kuwa ni pamoja na usalama wa ardhi, uhakika wa milki, kupunguza migogoro pamoja na nyaraka hiyo kutumika kama dhamana.

Zaidi ya wananchi 6000 katika vijiji 22 wamepangiwa matumizi bora ya ardhi katika maneo yao na kuwekewa mipaka ya kudumu ili kuepuka migogoro ya mipaka kwenye ardhi zao

Serikali kupitia halmashauri ya wilaya ya Serengeti, Shirika la Hifadhi la Taifa Serengeti (SENAPA) na Shirika la Frankfurt Zoological Society (FZS) kwa ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KFW) kupitia mradi wa utunzaji na uendelezaji wa Ikolojia ya Serengeti waliingia makubaliano ya pamoja kwa ajili ya kuwezesha uandaaji wa mpango wa matumizi ya ardhi ya vijjji vinavyopakana na maeneo yaliyohifadhiwa yanayounda ikolojia ya serengeti inayojumuisha hifadhi za taifa na mapori ya akiba.

Madhumuni ya mradi huo ni pamoja na kupunguza migogoro ya matumizi ya ardhi kati ya vijiji na eneo la hifadjhi , kutatua migogoro ya mipaka kati ya maneo ya kiutawala pamona na kutoa elimu ya uhifadhi na sheria mbalimbambalj  zinazosimamia mipango ya matumiZi ya ardhi nchini.

Read More

DRC yawa mwanachama kamili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki


Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo sasa ni mwanachama kamili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

DRC imeidhinishwa rasmi kuwa mwanachama wa saba wa EAC baada ya Christophe Lutundula, Naibu Waziri Mkuu Anayeshughulikia Masuala ya Nje ya Kongo DR kukabidhi nyaraka kwa makao makuu ya jumuiya hiyo ya kikanda huko Arusha, Tanzania.

Hatua ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuidhinishwa rasmi kuwa mwanachama kamili wa EAC ina maanisha kuwa, nchi hiyo sasa ina haki zote za nchi mwanachama wa jumuiya hiyo, na itafaidi mambo mengi kama wanachama wengine.

Baadhi ya mambo itakayofaidi DRC baada ya kupasishwa rasmi kuwa mwanachama kamili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ni kuruhusiwa raia wake kuingia katika nchi wanachama wa jumuiya bila viza.

Vile vile soko lake litapanuka kutokana na uagizaji na usafirishaji huru wa bidhaa hususan katika maeneo ya mashariki ya kanda hiyo ya Afrika, yanayotegemea bandari za Mombasa na Dar es Salaam. Aidha nchi hiyo sasa ina haki ya kuteua wanachama 9 wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) na majaji wa Mahakama ya Uadilifu ya jumuiya hiyo EACJ. 

Peter Mathuki, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki amesema mchakato wa DRC kujiunga na jumuiya hiyo umekamilika, na sasa ni rasmi nchi hiyo ni mwanachama kamili wa EAC.

Sudan Kusini ilikuwa nchi ya mwisho kukubaliwa kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki mwezi Machi mwaka 2016, kabla ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kukubaliwa kujiunga na jumuiya hiyo Machi mwaka huu.


Read More

Tuesday, July 12, 2022

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo July 12

Read More

Sunday, July 10, 2022

NECTA Yatangaza Matokeo ya Mitihani Kidato cha Sita Na Ualimu 2022


Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya mitihani ya kidato cha sita na ualimu kwa mwaka 2022 .

Matokeo hayo yametangazwa na Necta leo Julai 5, 2022.

==>>BOFYA HAPA KUTAZAMA MATOKEO


Read More

Orodha Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Na Kidato Cha Tano Awamu Ya Pili,2022


KATIBU Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Prof.Riziki Shemdoe anawatangazia wananchi wote kuwa orodha ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano awamu ya pili kwa mwaka 2022 imetoka.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Bi.Nteghenjwa Hosseah ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI). Bonyeza mkoa wako hapo chini kulingana na hitaji lako;

==>>BOFYA  HAPA  KUTAZAMA MAJINA

Read More

Nafasi Mpya za Kazi Serikalini,NGOs na Makampuni Binafsi


Kama unatafuta kazi kwa muda mrefu bila mafanikio, basi hii ni nafasi yako!! Hapa kuna  Nafasi za kazi zaidi ya 4800 zilizotangazwa wiki hii . Chagua unayoitaka hapo chini

_________

Read More

Kagame asema atagombea tena urais wa Rwanda 2024


Rais Paul Kagame wa Rwanda, ambaye amekuweko madarakani tangu yalipohitimishwa mauaji ya kimbari nchini humo mwaka 1994, amedokeza kuwa atagombea tena urais katika uchaguzi unaotazamiwa kufanyika 2024.

Alipoulizwa katika mahojiano na televisheni ya France 24 kama atawania tena kiti cha urais katika uchaguzi ujao, Kagame amesema: "Ninafikiria kugombea kwa miaka 20 mingine. Sina tatizo juu ya hilo". Rais huyo wa Rwanda ameongezea kusema, uchaguzi unahusu chaguo wanalofanya watu.

Kagame aliifanyia mabadiliko katiba ya Rwanda mwaka 2015 na hivyo kumfungulia njia ya kuweza kubaki madarakani hadi 2034.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 64 alishinda uchaguzi wa rais wa 2017 kwa asilimia 99 ya kura kulingana na matokeo rasmi.

Paul Kagame, alikuwa na umri wa miaka 36 tu wakati harakati yake ya Rwanda Patriotic Front (RPF) ilipowatimua Wahutu wenye misimamo ambao wanalaumiwa kuhusika na mauaji ya kimbari yaliyotokea kuanzia Aprili hadi Julai 1994 na kusababisha watu wasiopungua laki nane kuuawa, wengi wao  wakiwa ni Watutsi.

Licha ya kuandamwa na tuhuma za ukiukaji wa haki za binadamu, Rais wa Rwanda ametetea vikali rekodi ya serikali yake katika suala hilo pamoja na uhuru wa kisiasa alipohutubia mkutano wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola, Commonwealth uliofanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo Kikgali mwishoni mwa mwezi uliopita wa Juni.../


Read More

Uhuru Kenyatta: Nilikuwa tayari kuachia urais ili kulinda damu za Wakenya


Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amekiri kuwa alikuwa tayari kujiondoa katika kinyang’anyiro cha urais baada ya Mahakama ya Juu kufutilia mbali ushindi wake wa Agosti 9, 2017.

Rais Kenyatta amesema alikuwa tayari kuchukua hatua hiyo kuzuia umwagikaji wa damu ambao ungesababishwa na machafuko ya baada ya uchaguzi.

Kiongozi huyo wa Kenya aliyasema hayo alipokuwa akihutubia mamia ya viongozi wa kidini kutoka eneo la Mlima Kenya katika Ikulu ya Nairobi.

 “Mengi yamesemwa kunihusu. Baadhi ya watu wamekuwa wakidai kuwa nilitaka kurudi Gatundu baada ya Mahakama ya Juu kufutilia mbali ushindi wangu.

 “Ninathibitisha kwamba madai hayo ni ya kweli. Nilitaka kwenda nyumbani. Ikiwa kujiondoa kwangu kungeleta amani nchini, basi nilikuwa tayari kuondoka. Maisha ya binadamu ni muhimu kuliko wadhifa wa urais,” amasema Rais Kenyatta.

Naibu wa Rais wa Kenya, William Ruto aliwahi kuwaambia wazee wa Mlima Kenya katika kikao cha faragha kilichofanyika nyumbani kwake mtaani Karen, Nairobi, kuwa nusura ampige kofi Rais Kenyatta alipoonyesha dalili ya kutaka kujiondoa kwenye kinyang’anyiro cha urais mara baada ya ushindi wake kubatilishwa na Mahakama ya Juu.

Katika sauti iliyorekodiwa kisiri kutoka kwenye mkutano huo, Ruto anasikika akisema kuwa, alimlazimisha Rais Kenyatta kushiriki uchaguzi wa marudio uliofanyika Oktoba 26, 2017.

Wanasiasa wa muungano wa Azimio la Umoja wamekuwa wakitumia ufichuaji huo kumponda William Ruto katika kampeni zao, huku wakijaribu kumfanya Naibu wa Rais aonekane kama kiongozi mwenye uchu wa madaraka.

Alhamisi iliyopita, Ruto alijitetea kuwa hakuwa na nia ya kumpiga kofi Rais Kenyatta kama inavyodaiwa.

Hata hivyo Kenyatta alionekana kumshambulia Ruto kwa ‘kuwapotosha’ Wakenya kuwa “alitaka kuachana na urais ilhali wapinzani wake ndio wamekuwa wakidai kuwa alilenga kubadilisha Katiba kupitia mswada wa BBI ili asalia mamlakani”.

Rais Kenyatta amewataka viongozi wa kidini kutoka eneo la Mlima Kenya kutohadaiwa na propaganda za baadhi ya wanasiasa wakati huu Uchaguzi Mkuu unapokaribia.

Uchaguzi wa rais nchini Kenya umepangwa kufanyika Agosti 9 mwaka huu.


Read More

Rais Samia afanya uteuzi BASATA

Read More

Rais Samia ateua bosi mpya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More

NEC yamteua Tamima Haji kuwa Mbunge Viti Maalum CCM


 TUME ya Taifa ya Uchaguzi nchini (NEC) imemteua, Tamima Haji Abass kuwa Mbunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imefanya uteuzi huo kufuatia kikao chake cha  Julai 9, 2022 kwa kuzingatia matakwa ya ibara ya 78 (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 ikisomwa pamoja na kifungu cha 86A (6) na (8) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343.
 
Hayo yamebainishwa kupitia taarifa iliyotolewa  Julai 9, 2022 na Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC, Dkt.Wilson Mahera Charles.

Amesema, uteuzi huo umefanyika baada ya tume hiyo kupkea barua Mei 12, 2022 yenye Kumb. Na. CEB. 137/400/02A/10 kutoka kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyoandikwa kwa mujibu wa kifungu cha 37(3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343.

Barua hiyo ilitaarifu kuhusu uwepo wa nafasi wazi ya Mbunge wa Viti Maalum wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kutokana na kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Mheshimiwa Irene Alex Ndyamkama.



Read More

Arafat ashinda Makamu wa Rais Yanga, hawa ndio wajumbe watano


Mwenyekiti wa kamati ya Uchaguzi Yanga SC Malangwe Mchungahela ametangaza Arafat Haji kuwa ndio mshindi wa nafasi ya Makamu wa Rais wa Yanga kwa kura 545 dhidi ya Suma Mwaitenda aliyepata kura 234.

Kwa mujibu wa kura zilizopigwa nafasi ya wajumbe watano wa kamati ya Utendaji walioshinda ni Yanga Makaga, Seif Gulamali, Rogers Gumbo, Munir Seleman na Alexander Ngai.

Wajumbe na makamu wa Rais sasa wanaenda kuungana na Rais wa club Injinia Hersi ambaye mapema alipitishwa bila kupingwa kuwa Rais wa club hadi 2030.


Read More

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo July 10

Read More
End: