Marekani imesema inaondoa msaada wa dola bilioni moja kwa Afghanistan na kutishia kupunguza zaidi aina zote za ushirikiano na taifa hilo baada ya wanasiasa hasimu nchini humo kushindwa kukubaliana kuunda serikali mpya.
Uamuzi huo wa Marekani umetangazwa siku ya Jumatatu na waziri wa mambo ya kigeni wa nchi hiyo Mike Pompeo aliyefanya ziara ambayo haikutangazwa mjini Kabul.
Pompeo alifanya ziara hiyo kwa lengo la kukutana na wanasiasa hasimu nchini humo ambao ni rais Ashraf Ghani na Abdullah Abdullah ambao wote wamejitangaza kuwa marais baada ya uchaguzi uliozozaniwa wa mwaka uliopita.
Wakati wa ziara hiyo Pompeo alitumai ataweza kumaliza mkwamo wa kisasa uliopo lakini hakufanikiwa.
Katika taarifa yenye matamshi makali Pompeo amenyooshea kidole cha lawama wanasiasa hao wawili kwa kushindwa kufanya kazi pamoja hatua inayotishia kuuweka rehani mkataba wa amani utakaowezesha kumaliza mzozo wa muda mrefu nchini humo.
Mkataba wa amani kati ya Marekani na kundi la wanamgambo wa Taliban la nchini Afghanistan umetoa matumaini ya kumaliza ushiriki wa Marekani na majeshi yake nchini Afghanistan tangu ilipojitumbukiza kwenye mzozo huo mwaka 2001.
Credit: DW
Credit: DW
Loading...
Usipitwe na Habari Yoyote. Install Mpekuzi App kwenye Simu Yako Upate Habari Zetu kwa Wepesi Zaidi
==>>... << BOFYA HAPA Kui Install>>
Mgid
hapa
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )