Akizungumza katika mkutano na wanahabari jijini Nairobi waziri wa Afya Mutahi Kagwe amesema kwamba watu wengine wawili wamepoteza maisha yao kutokana na maambukizi ya virusi hivyo.
Amesema kwamba idadi hiyo inaongeza idadi ya watu waliofariki kutokana na ugonjwa huo kufikia 3. Kagwe ameongezea kwamba wagonjwa waliofariki wanatoka miji ya Nairobi na Mombasa.
Waziri huyo pia amepiga marufuku usafiri wa Wakenya kuelekea katika maeneo ya mashambani akionya kwamba huenda wakapeleka maambukizi ya virusi hivyo katika maeneo hayo.
Amesema kwamba serikali imewapima watu 662 katika kipindi cha saa 24 ambapo takriban watu 29 wamepatikana na virusi hivyo.
Kagwe amesema kwamba wagonjwa 28 kati ya wale waliopatikana na virusi hivyo ni raia wa Kenya huku mmoja akiwa raia wa DR Congo.
Waziri huyo pia amepiga marufuku usafiri wa Wakenya kuelekea katika maeneo ya mashambani akionya kwamba huenda wakapeleka maambukizi ya virusi hivyo katika maeneo hayo.
Amesema kwamba serikali imewapima watu 662 katika kipindi cha saa 24 ambapo takriban watu 29 wamepatikana na virusi hivyo.
Kagwe amesema kwamba wagonjwa 28 kati ya wale waliopatikana na virusi hivyo ni raia wa Kenya huku mmoja akiwa raia wa DR Congo.
Loading...
Usipitwe na Habari Yoyote. Install Mpekuzi App kwenye Simu Yako Upate Habari Zetu kwa Wepesi Zaidi
==>>... << BOFYA HAPA Kui Install>>
Mgid
hapa
Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )